Matthew 22:41-45
41 aWakati Mafarisayo walikuwa wamekusanyika pamoja, Isa akawauliza, 42 b“Mnaonaje kuhusu Al-Masihi? ▼▼ Al-Masihi maana yake ni Masiya , yaani Aliyetiwa mafuta.
Yeye ni mwana wa nani?” Wakamjibu, “Yeye ni mwana wa Daudi.” 43Akawaambia, “Inakuwaje basi kwamba Daudi, akinena kwa kuongozwa na Roho, anamwita Al-Masihi ‘Bwana’? Kwa maana asema, 44 d“ ‘Bwana alimwambia Bwana wangu:
“Keti mkono wangu wa kuume,
hadi nitakapowaweka adui zako
chini ya miguu yako.” ’
45Kama basi Daudi anamwita yeye ‘Bwana,’ awezaje kuwa mwanawe?”
Copyright information for
SwhKC